SiasaMarekani
Trump asema "SAWA" Zelensky kuzuru Marekani
26 Februari 2025
Matangazo
Akizungumza na waandishi wa habari kwenye ofisi yake ya Oval, Trump amesema yuko tayari kukutana na Zelensky ambaye kulingana naye amesikia anakwenda Washington siku ya Ijumaa. "Ndiyo, nasikia anakuja Ijumaa, sina tatizo. Na atapenda kusaini na mimi. Na ninajua kwamba ni makubaliano makubwa. Na nadhani Wamarekani wanafurahia kwa sababu, Biden alikuwa anatapanya tu pesa kama pipi. Haya ni makubaliano makubwa. Yanaweza kufikia dola trilioni 1 na ni madini adimu sana duniani." Amesema Trump.
Kulingana na Marekani na ripoti za vyombo vya habari, Ukraine tayari imekubaliana na toleo la mwisho la rasimu ya makubaliano hayo yaliyopendekezwa na Marekani siku ya Jumanne.