SiasaMarekani
Trump asema mengi yamekubaliwa kuhusu Ukraine
18 Machi 2025Matangazo
Trump ameyasema haya kuelekea mazungumzo yake kwa njia ya simu na Rais wa Urusi Vladimir Putin hii leo, kuhusu kuvimaliza vita vya Ukraine.
Katika ujumbe aliouandika kwenye mtandao wa kijamii, Trump amesema anayasubiri kwa hamu mazungumzo yake na Putin.
Soma pia: Ramaphosa: Kuimarisha uhusiano na US ni kipaumbele chetu
Ikulu ya Kremlin hapo jana ilithibitisha kwamba Putin atazungumza na rais huyo wa Marekani.
Trump amesema ardhi na viwanda vya umeme ni mambo yanayozingatiwa katika mazungumzo ya kufikisha mwisho vita hivyo.