Trump asema Crimea itasalia chini ya udhibiti wa Urusi
25 Aprili 2025Trump ameongeza kuwa Rais wa Ukraine, Volodymyr Zelensky, anaelewa hali halisi kwamba Crimea imekuwa chini ya udhibiti wa Urusi kwa muda mrefu, na kwamba wakaazi wa eneo hilo wengi huzungumza lugha ya Kirusi.
Mjumbe wa Marekani akutana na Putin kujadili vita vya Ukraine
Wakati hayo yakijiri, Urusi imeendelea na mashambulizi yake ndani ya Ukraine. Katika tukio la hivi karibuni, bomu lililovurumishwa na jeshi la Urusi limelipua jengo la makazi katika mji wa kusini-mashariki mwa Ukraine, na kuua watu watatu huku wengine 10 wakijeruhiwa.
Trump atoa wito kwa Urusi kusitisha mashambulizi Ukraine
Maafisa wa eneo hilo wamethibitisha mashambulizi hayo, ikiwa ni siku moja tu baada ya Trump kumlaumu Rais wa Urusi, Vladimir Putin, kwa mashambulizi makali ya makombora na droni yaliyoilenga mji mkuu wa Ukraine, Kyiv.