JangaAsia
Tetemeko la ardhi laporomosha jumba la ghorofa Bangkok
28 Machi 2025Matangazo
Hayo yamesemwa na polisi na madaktari baada ya mji huo kutikiswa na tetemeko kubwa la ardhi.
Kwa mujibu wa taasisi ya utafiti wa kijiologia ya Marekani ( USGS) ni kwamba tetemeko hilo kubwa la ardhi la ukubwa wa kipimo cha richter 7.7, limesababisha daraja na majengo kadhaa kuanguka katika nchi hiyo ya kusini-mashariki mwa Asia.
Mji wa Bangkok ulitikiswa kwa dakika kadhaa na tetemeko hilo na kusababisha watu kutoka nje ya nyumba zao kwa hofu huku katika miji mingine watu walikuwa mitaani na maelfu ya wengine wakikimbia.
Watoa misaada walimwagwa barabarani mara moja kuwaelekeza watu kutoka nje ya nyumba zao na kwenda kwenye maeneo ya wazi huku wagonjwa nao wakitolewa hospitali na kuwekwa nje.