Tetemeko la ardhi Iran: -Marekani yatuma misaada
29 Desemba 2003Wanajeshi wa Kimarekani na wenzao wa Iran wameshirikiana bega kwa bega kubakua shehena ya misaada iliosafirishwa na ndege ya uchukuzi ya Marekani vikiwemo vifaa vya tiba, chakula na maji. Kadhalika ndege za kijeshi za Jordan zikiwa na mahema maalum yanayotumiwa kama hospitali za dharura na vifaa,pamoja na misaada mengine zilituwa nchini Iran mapema alfajiri ya leo. Kiongozi mkuu wa kidini nchini humo Ayatollah Ali Khamenei aliwasili mjini Bam leo kujionea hasara iliodababishwa na janga hilo pamoja na juhudi zinazoendelea, huku kiwa na ulinzi mkali kuwahi kuonekana mini humo . Baadae leo abatarajiwa pia kufika eneo hilo Rais Mohammad Khatami.
Kwa upande mwengine majeshi ya usalama yamezifunga njia zinazoelekea mjini humo kwa aina yote ya magari isipokua tu malori na magari yanayosafirisha misaada na wafanyakazi wa shughuli hizo. Hatua hiyo ina lenga kuzuwia mtafaruku na visa vya uporaji wa misaada inayohitajika kwa dharura, sawa na hali iliojitokeza hapo jana, wakati baadhi ya magari yalipowasili eneo hilo yakiwa tayari yamesafishwa na waporaji.Maafisa wamelaumu wakaati wa vijiji vya karibu na Bam . sambamba na magari , hadi sasa zaidi ya helikopta 500 zimejiunga na shughuli za usafirishaji misaada hadi Bam, tokea Ijumaa lilipotokea tetemeko hilo , ambalo limeuharibu kabisa mji huo wa kihistoria.
Taarifa ya serikali ilisema waliuwawa ni 22,000 lakini nyengine zinasema huenda waliouwawa ni hadi watu 30,000. Zaidi ya 2,000 wameokolewa kutoka vifusi vya majumba yalioporomoka. Wengi wa walionusurika na kulazimika kubakia mjini humo wanaishi katika mahema chini ya baridi kali. Wengine 12,000 wamesafirishwa kwa ndege na kupelekwa katika mikoa mengine.