Takriban watu 4 wauawa katika shambulizi la RSF nchini Sudan
12 Julai 2025Matangazo
Katika taarifa, shirika hilo la madaktari limesema kikosi hicho cha RSF kilishambulia kwa mizinga vitongoji vyenye idadi kubwa ya watu, wengi wao wakiwa wakimbizi katika eneo la El-Obeid, mji mkuu wa jimbo la Kordofan Kaskazini, Alhamisi usiku, na kuwauwa huku wengine wakijeruhiwa.
Mashirika ya misaada yaonya kuhusu mashambulizi dhidi ya hospitali Sudan
Wakati huo huo, shirika la kimataifa la misaada ya kibinadamu la Mercy Corps, limesema kuwa eneo la Kordofan limekuwa kitovu cha vita vinavyoendelea huku mapigano yanayoendelea kaskazini, kusini, na magharibi mwa Kordofan yakitatiza upatikanaji wa chakula, maji, huduma za matibabu na barabara salama.