Syria yatangaza kusitisha mapigano ya kidini
15 Julai 2025Matangazo
Qasra amesema makubaliano hayo yamefikiwa siku moja baada ya mapigano ya kidini kati ya jamii za Bedui na Druzekuwaua takribani watu 100.
Waziri Mkuu wa Israel, Benjamin Netanyahu na Waziri wa Ulinzi, Israel Katz katika taarifa yao ya pamoja walidai Israel ilisaidia kuzuia utawala wa Syria kuwadhuru jamii ya wachache wa dini ya Druze, na kuhakikisha wapiganaji wanapokonywa silaha katika eneo hilo lililopo karibu na mipaka ya Syria.
Nchini Israel, jamii ya Druze huonekana kama watiifu na mara nyingi wanatumika katika jeshi.