Syria yakanusha kuhusika na mashambulizi dhidi ya Israel
4 Juni 2025Syria imelaani shambulizi hilo na kulitaja kuwa ukiukaji mkubwa wa uhuru wake unaozidisha wasiwasi katika eneo hilo.
Israel yafanya mashambulizi mjini Damascus
Katika taarifa yake, wizara ya mambo ya nje ya Syria imekanusha kuishambulia Israel na kusema haiwezi kuthibitisha ikiwa roketi zilirushwa kuelekea Israel na kuzilaumu pande nyingine kwa kujaribu kuliyumbusha eneo hilo.
Israel yawashambulia wapiganaji wanaowalenga jamii ya wachache ya Druze
Vyombo vya habari vya Israel vimesema roketi hizo ni za kwanza kurushwa kutoka Syria kuelekea katika ardhi ya Israel tangu kuanguka kwa kiongozi wa muda mrefu Bashar al-Assad mwezi Desemba, huku makundi mawili yasiyojulikana yakidai kuhusika.
Waziri wa ulinzi Israel Katz amemlaumu moja kwa moja kiongozi wa Syria, Ahmed al-Sharaa.