Syria yaituhumu Israel kufanya kampeni ya kuidhoofisha
3 Aprili 2025Matangazo
Mamlaka katika mkoa wa kusini mwa Syria wa Daraa zimesema raia 9 wameuwawa na wengine kadhaa kujeruhiwa katika mashambulizi ya anga ya Israel karibu na mji wa Nawa.
Israel kwa upande wake imesema ilikuwa inajibu mashambulizi ya risasi kutoka kwa watu waliokuwa wamejihami wakati wa operesheni ya kusini mwa Syria na ikamtahadharisha Rais wa muda Ahmed al-Sharaa kwamba kutakuwa na adhabu kali endapo usalama wa Israel utatishiwa.