JangaSudan
Sudan: Ndege ya kijeshi yaanguka na kuwauwa zaidi ya watu 40
26 Februari 2025Matangazo
Karibu watu 46 wamekufa baada ya ndege ya kijeshi ya Sudan kuanguka jana Jumanne katika mji wa Omdurman.
Kulingana na maafisa wa Afya na jeshi, wanajeshi na raia walikufa katika eneo la ajali ingawa hawakutaja idadi kamili na wala chanzo cha ajali hiyo.
Ndege hiyo ya Antonov ilianguka wakati inapaa kutoka kwenye uwanja wa ndege wa jeshi la anga la Wadi Sayidna kaskazini mwa Omdurman, taarifa ya jeshi imesema.
Wizara ya Afya imesema karibu watu hao 19 wamekufa, na miili yao ilipelekwa hadi Hospitali ya Nau, mjini Omdurman. Hospitali hiyo pia imepokea majeruhi watano.