Starmer kuwakutanisha viongozi wa Ulaya juu ya Ukraine
1 Machi 2025Kabla ya mkutano huo wa Jumapili (Machi 2) Starmer atakuwa na kikao kwa njia ya simu la mataifa ya Baltiki, kabla ya kukutana na Rais Volodymyr Zelensky wa Ukraine jijini London.
Ofisi yake imesema Starmer atatumia mikutano hiyo kusukuma mbele ajenda ya mpango wa Ulaya kwa Ukraine, ambao unahusisha kile wanachokiita "amani ya kudumu na ya haki kwa mamlaka na mustakabali wa Ukraine."
Soma zaidi: Viongozi wa Ulaya waafikiana kuhusu kuimarisha usalama wao
Viongozi wa Ufaransa, Ujerumani, Denmark, Uturuki, Muungano wa Kijeshi wa NATO na Umoja wa Ulaya wamealikwa kwenye mkutano huo wa kilele wa Jumapili.
Starmer, ambaye juzi alikuwa mjini Washington kukutana na Rais Donald Trump, amewaalika pia viongozi wa Uholanzi, Norway, Poland, Uhispania, Finland, Sweden, Romani na Jamhuri ya Czech kwenye mkutano huo.